Mtu aliyetuhumiwa kujaribu kuiba pikipiki aina ya Bajaj maeneo ya Coco Beach Dar es Salaam akiwa tahabani baada ya kupata kipigo cha mbwa mwizi maeneo ya
Msasani jirani na Hospitali ya CCBRT hivi karibuni. Kwamujibu wa mashuhuda wa tukio hilo kijana huyo alikubwa na mkasa huo alipokuwa katika harakati za kukimbia na inadaiwa alikuwa na hirizi inayomsaidia kuendelea kupumua. Askari wa Kituo cha polisi cha Oysterbay walifanikiwa kumpeleka Hospitali ya Mwananyamala na tutawajuza kama anaendelea na hali gani. Kwa mujibu wa askari wa Kituo hicho wamethibitisha kumfikisha hospitalini na kwa kuwa hakuna anayemtuhumu baada ya kupata kipigo kikali watafanya mchakato wa kumlinda mpaka atoke hospitalini.
No comments:
Post a Comment