Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira imesema Serikali imekuwa ikitoa maagizo ya kubadilishwa kinyemela mipaka ya Hifadhi ya Taifa ya Arusha.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, James Lembeli alisema
mwaka 2005 Serikali kupitia gazeti la Serikali namba 280, iliongeza
mipaka ya hifadhi kwa kuingiza msitu wa asili na ule wa kupanda.
Lembeli alisema kwa mujibu wa taarifa walizonazo,
Serikali ya awamu ya nne iliamua kubatilisha uamuzi wa Serikali kwa
kuliagiza Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) kurekebisha mipaka yake.
Lembeli ambaye pia ni Mbunge wa Kahama, alikuwa
akizungumza na waandishi wa habari juzi baada ya wajumbe wa kamati yake
kutembelea hifadhi hiyo iliyopo nje kidogo ya mji wa Arusha.
Alisema kwa utaratibu iwapo Serikali ilikuwa
inaona ilifanya makosa katika tangazo lake namba 280, mabadiliko hayo ya
mipaka yalitakiwa yapelekwe bungeni kama azimio ili Bunge liamue.
Alisema kutokana na ubabaishaji huo, kuanzia
wakati huo (mwaka 2005) mpaka sasa, yale maeneo ambayo Tanapa iliambiwa
iyaache yanasimamiwa na chombo ambacho hakina mamlaka kisheria.
Kamati hiyo imeagiza Wizara ya Maliasili na Utalii
kuwasilisha taarifa kwa kamati ili kuthibitisha suala hilo, ikiwezekana
kuifahamisha aliyehusika kutoa maagizo hayo kwa Tanapa.
“Tungependa kufahamu aliyetoa maagizo hayo kwa
Tanapa na kuwafanya washindwe kutekeleza sheria ile kupitia gazeti la
Serikali, kuruhusu wananchi kufanya watakavyo ndani ya hifadhi,”
alisema.
Wakati huohuo, kamati hiyo imesema anguko la
shughuli za uhifadhi na utalii maeneo mbalimbali yaliyotengwa,
zinatokana na tabia ya kuingiza siasa katika shughuli za hifadhi.
Lembeli alisema kuna dalili za siasa kunyemelea uhifadhi na
alitahadharisha kuwa,
uhifadhi ni sayansi hivyo siasa haina nafasi badala yake utaalamu ushike hatamu.
uhifadhi ni sayansi hivyo siasa haina nafasi badala yake utaalamu ushike hatamu.
No comments:
Post a Comment