Huenda ni jambo lisilowezekana mtu kusema kwamba anataka kuwa na maisha
ya shida, kama atakuwepo basi huenda mawasiliano kwenye ubongo yakawa
yameingizwa na shida; tunaweza kusema hawa ni aina ya watu maalumu
wanaohitaji msaada maalum...teh!teh!teh!
Unapozungumza na watu karibu wote duniani, kila mtu atakwambia ninachotaka ni kuwa na maisha bora.
Huenda
ni jambo lisilowezekana mtu kusema kwamba anataka kuwa na maisha ya
shida, kama atakuwepo basi huenda mawasiliano kwenye ubongo yakawa
yameingizwa na shida; tunaweza kusema hawa ni aina ya watu maalumu
wanaohitaji msaada maalum...teh!teh!teh!
Unaweza kuringa una shahada,
stashahada na elimu zingine, bado ukawa unachapwa bakora na maisha kama
hutakuwa makini; Kusoma sana au kidogo, kuwa na rafiki waliofanikiwa au
wasiofanikiwa, kwenda nje ya nchi au la, au kuzaliwa familia maskini au
tajiri, bado sio tiketi ya kukufanya uwe na maisha bora.
Msingi wa
kufanikiwa ni kuthubutu kufanya jambo fulani, kwa mfano kufungua mradi
na mambo mengine kama haya. Kuna watu kwa mfano unaweza kuona anakata
tamaa kwa sababu labda amezaliwa katika familia maskini, kitu ambacho
sio sahihi. Msingi wa kuwa na maisha bora ni kufanya kazi kwa bidii na
zaidi ni kuishi kwa malengo; Usiishi tu ili mradi siku zinakwenda mbele.
Kwa chochote unachokifanya, kifanye baada ya kutafakari na kuangalia
faida au hasara yake.
Katika kitabu changu cha mwongozo wa namna ya
kutengeneza bidhaa zikiwemo sabuni, mishumaa, vyakula vya kuku nk,
nilisema maisha yanatuhitaji kuwa waangalifu na wanadamu wanaotunguka,
lakini pia ni lazima tubuni miradi mingi zaidi ili tuweze kufanikiwa
kuwa na maendeleo.
Kuna mwingine hata ukimwangalia sura yake
anaonekana wazi kabisa kwamba hana furaha, unapomwambia kwamba mambo
yangu yanakwenda safi. Furaha ya watu walio wengi ni kusikia unaishi
maisha ya kawaida, au unaishi maisha ya shida.
Kwa bahati mbaya sana,
siku hizi hadi baadhi ya wazazi wamekuwa wabaya kwa watoto wao, kuna
wengine kwa mfano hajui ni kwa vipi unaendesha gari, unaishi nyumba
nzuri, badala yake anapokuona unaendesha gari zuri anakuja juu na
kulalamika kuwa mbona huwasaidii.
Ambacho nataka kusisitiza katika
makala haya ni kwamba mafanikio yako yanatokana na akili yako uliyonayo,
ndio maana wengine wamekuwa wakisema kuwa ‘ugumu wa maisha ndio kipimo
cha akili’.
Wengi wanapingana na msemo huu, lakini ndio ukweli
wenyewe kwamba hali ya maisha ambayo unayo, ndio hasa inayoeleza hali ya
uwezo wa kufikiri. Endapo utatumia akili, hisia na imani yako kwa
busara na kufanyia kazi, ni lazima maisha yako yatakuwa na mabadiliko
makubwa.
Kama wewe ni mwanaume, hebu tuseme ule ukweli unafanya ngono
na wanawake wangapi? Unawahonga kiasi gani au unatumia kiasi gani kwa
ajili ya mambo yasiyo na maana? Jibu unalo, kama unapanda fedha zako
kwenye kuhonga, kisha unatarajia maendeleo, bila shaka akili yako haiko
sawa; watu huvuna wanachopanda, si ndiyo?
Katika kitabu cha tiba ya
ndoa ambacho ni maalum kuhusu namna ya kuishi kwenye ndoa nilifafanua
namna gani wanapaswa kufanya ili mwenzi wako asikuchoke au namna gani
ufanye ili kuifanya ndoa yako iwe ya maana; Mtu huvuna kile alichopanda,
si ndio jamani? Kama unaelekeza fedha nyingi kwenye kitu fulani,
hakuna
ubishi kwamba mwisho wa siku utavuna matunda ya kile kitu ambacho
umewekeza fedha zaidi.
Unaweza kumficha mkeo asijue una wanawake
ulionao, lakini amini ninachokwambia hakuna ujinga uliopitiliza duniani
kama kufanya ngono hovyo na kukubali kutumiwa kama mashine ya kutolewa
fedha;
badala ya kuendeleza kwako unakuwa mjinga wa kuhonga wanawake
kisa wanakupa nanilihii.
Tangu umeanza kufanya umepata nini? Jibu
unalo mwenyewe; amini ninachokwambia ni ngumu kwako kufanikiwa kama
unaendekeza mambo ya ajabu. Je, maisha yako unayaendeshaje? Chukua
hatua.
No comments:
Post a Comment