WanaCCM msiwe na shaka, tutavuka kwa nguvu zetu... wingi wenu huu unanipa faraja kuwa katika safari yetu na kwa kumte gemea Mungu tutashinda ...Tulifurahi pamoja, tulihuzunika pamoja na tutashinda pamoja.”
Tangu Lowassa atoe kauli kuhusu ‘safari yake ya matumaini’ zimetolewa kauli nyingi za ama kupingana naye au kumsapoti katika safari hiyo, hivyo kuhatarisha mshikamano wa CCM.
Nguvu ya makundi ya watu wanaotajwa kuwania urais kupitia Chama
Cha Mapinduzi (CCM) zinaendelea kukitikisa chama hicho huku makada wake
wakitoa angalizo wakiutaka uongozi wa juu wa kuchukua hatua haraka za
kinidhamu kwa wahusika.
Wiki iliyopita wanachama wa chama hicho wanaodaiwa
kutoka katika kambi tofauti zinazoisaka nafasi ya urais waliibuka na
kutoa kauli zinazoonekana wazi kupigana vijembe, kila upande ukiuponda
mwingine kuwa unavunja kanuni na katiba ya chama hicho.
Malumbano hayo ya makada wa CCM yanayoonekana
dhahiri kuchagizwa na makundi pamoja na wafuasi wa vigogo wanaousaka
urais kupitia chama hicho.
Ingawa makundi yanayosaka urais kupitia chama
hicho ni mengi, ni kundi moja tu linalomuunga mkono aliyekuwa waziri
mkuu, Edward Lowassa ndilo linaloonekana dhahiri kupigiwa kelele kwa
kutajwa kwa majina bila kificho, hasa baada ya kauli yake kuwa ameanza
safari, aliyoitoa mbele ya wageni wakati wa kuadhimisha mwaka mpya 2014.
Kutokana na kauli hiyo na mambo mengine, Katibu wa
Uhamasishaji na Chipukizi wa UV-CCM, Paul Makonda aliibuka na
kumshambulia Lowassa, suala ambalo limeyaibua makundi mengine, baadhi
yakiunga mkono kauli ya Makonda na mengine yakiibeza na kumshushia
tuhuma za kuvunja kanuni za chama.
Mmoja kati ya waliojitokeza ni Makamu Mwenyekiti
mstaafu wa CCM, John Malecela ambaye ameonyesha waziwazi kutofautiana na
mipango na mikakati ya Lowassa.
Malecela anamuunga mkono Makonda, kwa kauli yake,
ikiwamo kwamba Lowassa anafadhili mikakati ya kupingana na juhudi za
sekretarieti ya CCM chini ya Katibu Mkuu, Abdulrahaman Kinana na Katibu
wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.
Wakati Makonda na Mzee Malecela wakitoa tuhuma
hizo, makundi mbalimbali ya Jumuiya ya Vijana UVCCM nao wameibuka na
kumshutumu Makonda kuwa aliyoyasema ni maoni yake na siyo msimamo wa
Jumuiya hiyo.
Kauli hiyo ya Makonda imeibua malumbano baina ya
viongozi wa jumuiya hiyo, wengi wakimshutumu kwa “kutumiwa kumchafua
Lowassa” na kwamba kauli aliyoitoa ni ya kwake na idara yake, wala
isihusishwe na Umoja wa Vijana wa CCM.
Baadhi ya waliojibu ni pamoja na wajumbe wa
Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) kupitia kundi la vijana, Jonas Nkya na
Ramadhani Kimwaga, pamoja na Mjumbe wa Baraza Kuu la jumuiya hiyo Mkoa
wa Mbeya, Adam Mwakalinga.
Vijana hao kwa nyakati tofauti wanasema
wamehuzunishwa na matamshi ya Makonda akimshutumu Lowassa na kutamka
kuwa umoja huo hautaki kuingizwa katika masuala binafsi ambayo yanaweza
kukigawa chama na jumuiya zake.
Mwakalinga anasema Makonda anapaswa kufanya kazi
ya idara yake ya watoto badala ya kukurupuka na kutaka kuwaaminisha
Watanzania kuwa Edward Lowassa si kiongozi mzuri huku akijua wananchi
wenyewe na hata wapinzani wanaona uthubutu wake katika maendeleo hasa
kwa vijana.
No comments:
Post a Comment