Thursday 2 May 2013

Nini chanzo cha baadhi ya vijana ambao wamefikia umri wa kuoa au kuolewa kuchelewa kuingia kwenye ndoa??


 

Kuna baadhi ya vijana ambao wanatamani kuingia katika ndoa lakini kuna baadhi ambao wanasema kwamba ,,bado nipo nipo kwanza,, na hii ni kwa wanaume na wanawake,,katika uchunguzi wangu nimeona kwamba vijana wengi wanachelewa kuoa au kuolewa kutokana na kuogopa majukumu kwani anaona bado hajajipanga vizuri, wengine ni kushindwa kujiamini anaogopa kuingia kwenye ndoa kwa hofu ya kukosa uhuru anaoutaka katika mambo yake ya starehe,,

 Wengine kutokana na kulazimishwa na wazazi kuoa au kuolewa na wachumba watakaowachagua wao  na kikubwa pia ni hali duni ya maisha kwani kuna mwingine anatamani kuoa lakini anaona kipato chake ni kidogo kufanya hivyo.

 Jamani mapenzi ni zaidi ya kipato ulichonacho kwani unaweza kuamua kuingia kwenye ndoa na huku mkiwa katika hali duni ya maisha,,baadae mkafanikiwa kwa juhudi zenu binafsi na kwa ushirikiano kati ya mke na mume muhimu ni kujiamini na kujitambua.....

No comments:

Post a Comment