Friday 1 November 2013

"SITASAHAU KAMWE JINA ALILOKUWA AKINIITA BABA..." WEMA SEPETU



WEMA Isaac Sepetu ‘Madam’ amefunguka kuwa kamwe hatasahau jina la Miss World ambalo marehemu baba yake, mzee Isaac Abraham Sepetu alikuwa akimuita. Akizungumza na mwanahabari wetu wakati wa kuaga mwili wa baba yake nyumbani kwao, Sinza-Mori jijini Dar, Jumanne iliyopita, Wema alisema baba yake alikuwa akimuita jina hilo kama utani kutokana na masuala ya urembo aliyokuwa akiyafanya hivyo alipofariki dunia jina hilo ndiyo kumbukumbu yake ya muhimu.

Marehemu Balozi Isaac Sepetu
“Sitalisahau jina la Miss World, baba ndiye alikuwa akiniita hivyo kila nilipokutana naye. Aliponiita hivyo nilikuwa nikifurahi sana,” alisema Madam. Mwili wa baba Wema ulisafirishwa Jumatano (jana) kuelekea visiwani Zanzibar kwa ajili ya mazishi.

No comments:

Post a Comment