Wednesday 22 January 2014

Mwinjilisti adaiwa kumuua mkewe

Inaonekana lengo lilikuwa kumteketeza kabisa mkewe.”mama na zile kuni kwenye tanuri”alisema Matei

Mwinjilisti wa Kanisa la Anglikana Kijiji cha Gama, wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani, anadaiwa kumuua mkewe kwa wivu wa mapenzi, kwa kumpiga na panga kichwani kisha kumfukia chini ya magogo aliyoandaa kwenye tanuri la mkaa porini.


Mwinjilisti huyo ambaye ni mkazi wa kijiji hicho, licha ya kazi ya kueneza Injili pia ni mkulima na anajishughulisha na shughuli za kuchoma mkaa porini.
Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Ulrich Matei alithibitisha tukio hilo na kwamba mwanamke aliyeuawa ni Mboni Patrick (28) mkazi wa kijiji hicho.
Matei alisema siku ya tukio Januari 20, saa 10:00 jioni Mwinjilisti huyo anadaiwa alitoka nyumbani akiwa na mkewe huyo na mtoto wao, Sabina Gabriel (10) kuelekea porini kukata miti ya kuandaa mkaa.
Matei alisema baada ya kukamilisha kukata miti, wanandoa hao walimtuma mtoto kurejea nyumbani kupika chakula ili wakimaliza kuwasha moto wakale.Alisema kuna dalili kuwa wakati mtoto anaondoka ndipo mume alipochukua panga na kumkata mkewe upande wa kulia kichwani, hivyo kuvuja damu nyingi.
“Baada ya kutekeleza mauaji hayo, baba huyo alichukua mwili na kuuweka katika tanuri walilokuwa wameliandaa kwa ajili ya mkaa na kuulaza chini, kisha kujaza magogo yote waliyokata na kuanza kuwasha moto,” alisema Matei na kuongeza:
“Inaonekana lengo lilikuwa kumteketeza kabisa mkewe.”mama na zile kuni kwenye tanuri”alisema Matei.
Kamanda huyo alisema muda mfupi mtoto aliyetumwa nyumani kupika alirudisha majibu porini ya chakula kuwa tayari lakini hakuwakuta wazazi wake na alianza kuita huku na kule bila mafanikio na ghafla ndipo alipoona damu nyingi imetapakaa jirani na tanuri na kufatilia akaona mkono ukichungulia kwenye tanuri la mkaa, huku damu ikichuruzika eneo hilo.
Alisema hali hiyo ilimpelekea mtoto kupiga yowe na kukimbilia kijijini na ndipo wanakijiji wakajitokeza na kuanza kuelekea eneo la porini na kukuta mwili wa mama huo ukiwa umefukiwa chini ya magogo ya mkaa kwenye tanuri huku ikivuja damu nyingi wakautoa na kuanza msako wa baba ambapo walimkuta ameshakufa kwa kujinyonga na mwili wake ulikua bado ukining’inia juu ya mti umbali wa mita 500 .
“Uchunguzi wetu wa awali ni kuwa Muinjilisti huyo hivi karibuni alipata taarifa kuwa mke wake ana mahusianao na mtu mwingine hali ambayo ilimuingizia msongo wa mawazo na bila ya kufatilia ndipo alipokubwa na shetani huyo na kuchukua hatua hiyo, kwa hiyo kiujumla sababu ya hili tukio ni wivu wa “alisema Matei.

No comments:

Post a Comment