
Katibu wa chama cha Mapinduzi wilaya ya Mbinga Anastasia Amasi akionyesha sehemu iliyoanzia moto kuwaka na kukamata pazia.
Katibu
 wa chama cha Mapinduzi wilaya ya Mbinga Anastasia Amasi anayeonekana 
katika picha akitoa  maelezo kwa nje ambapo walimwaga mafuta aina ya 
petroli dilishani na kuwasha moto 
WATU
  wasiojulikana wamechoma moto jengo la ofisi ya Chama cha Mapinduzi  
wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma..
  
Akithibitisha
  kutokea kwa tukio hilo katibu wa chama cha Mapinduzi wilaya ya Mbinga 
 Anastasia Amasi amesema kuwa tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Juni
  21 mwaka huu ambapo watu wasiojulikana walichoma moto moja ya jengo la
  ofisi za chama hicho wilayani humo  .
Moto huo ulielekelezwa katika  
chumba cha ofisi ya katibu ambapo walivunja vioo na kuchoma moto mapazia
  lakini kabla hawajachoma vitu vilivyokuwemo ndani walikimbia na kuacha
  dumu lililokutwa likiwa na mafuta aina ya petroli.
  
Alisema
  kuwa mpaka sasa hakuna hisia zozote zinazohusiana na tukio hilo ingawa
  uongozi wa chama cha mapinduzi wilayani humo umeshatoa taarifa kwenye 
 vyombo ya ulinzi na usalama ambavyo vinaendelea na uchunguzi wa tukio  
hilo.
  
Katika
  hatua nyingine , hali ya sintofahamu imejitokeza katika uchaguzi wa  
viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Mbinga baada ya halmashauri hiyo  
kugawanywa na kuzaliwa kwa halmashauri mpya ya wilaya Nyasa kwa kuibuka 
 kwa vitendo vya hujuma vinavyodaiwa kufanywa dhidi ya  mgombea mmoja wa
  nafasi ya mwenyekiti jina lake kuenguliwa katika mazingira ya  
kutatanisha na kuzua maswali mengi miongoni mwa madiwani wa halmashauri 
 pamoja na wananchi na kutaka uchaguzi huo usifanyike mpaka majina yote 
 matatu ya wagombea yawepo.
  
Mmoja
  wa wananchi wa halmashauri hiyo ya wilaya ya Mbinga ambaye pia ni  
katibu mwenezi wa chama cha mapinduzi  wa kata ya Mbinga mjini Monika  
John alisema kuwa hizo ni dalili za kuwepo kwa njama za wazi za kupanga 
 safu ya uongozi ambao siyo chaguo la walio wengi bali ni chaguo la  
baadhi ya viongozi wa halmashauri hiyo kwa masilahi yao.
  
Akizungumzia
  hali hiyo katibu wa chama cha mapinduzi wilaya ya Mbinga alisema kuwa 
 uteuzi wa wagombea wa nafasi hizo hufanywa kwa kuzingatia kanuni za  
chama na wenye jukumu la mwisho  la uteuzi ni uongozi wa chama ngazi ya 
 mkoa  na yeye si msemaji wa maamuzi ya ngazi mkoa ingawa amepokea 
tarifa  ya kusitishwa kwa uchaguzi huo mpaka taarifa nyingine 
itakapotolewa na  ofisi ya chama ngazi ya mkoa.
No comments:
Post a Comment