Wednesday 20 November 2013

KITENGE: Vazi ambalo kamwe haliwezi kumuangusha mvaaji

Vazi la kitenge, ni moja ya mavazi mashuhuri sana ambalo asili yake ilikuwa ni mwambao wa pwani ya Afrika ya Mashariki, kabla ya kuanza kusambaa umaarufu wake katika bara zima la Afrika na hatimaye duniani hivi sasa.


Ni vazi ambalo kwa ujumla wake linaweza kumpendeza kila mtu na kila rika.Kuanzia wanaume hadi wanawake, wazee hadi watoto, ni vazi ambalo kwa hakika linamtoa kila mmoja wao.

Iwe harusini au msibani, iwe kwenye hafla za kiserikali au shughuli za kawaida za kijamii, hakika vazi hili ni la kipekee na ambalo haliwezi kumuangusha mvaaji.

Hebu cheki baadhi ya mishono ya vazi hili adhimu na si mbaya nawe ukajaribu siku moja kutokelezea katika vazi hili




No comments:

Post a Comment