Thursday 21 November 2013

Ukiwa chumbani na mwandani wako, hebu mpe mambo haya.....

Si siri, mapenzi ni hatua ambayo kila mtu hutamani kuipitia. Na leo napenda nizungumzie faragha, yaani sehemu ambayo mnaweza kupeana raha za dunia bila tabu. Kabla ya kuwa faragha nadhani mlipeana miadi mpaka kukutana kwenu faragha, sasa basi unapokwesnda katika makutano yenu ya kuliwazana, unatakiwa uwe umejiandaa vya kutosho. Sina maana ya kubeba pesa kwa ajili ya mpenzio,maana kuna wasichana wengine bwana bila pesa hawajapeana ma-vitu.
Unaweza kujianda kuanzia mavazi, mwili na urembo hasa kwa wasichana. Nikizungumzia mavazi, namaanisha kuanzia nguo za ndani, kuwepo safi nguo za ndani hupendeza na kumvutia mwandani wako, sio unaenda kwa mwandani wako huku umevaa nguo ya ndani karibu wiki. Haipendezi hata kidogo na utaanza kumboa mwenzio.
Hakikisha nguo zako safi na zitamvutia zaidi, pia nguo laini na nyepesi humfanya aweze kukupapasa atakavyo kwani utakapovaa nguo ya kubana ama nzito inaweza kumnyima uhuru wakati mkiwa katika mwanzo wa faragha yenu. Wanaume wengi wamekuwa wakiudhiwa na wapenzi wao wanaovaa nguo zinazowabana sana wanapokuwa faragha. Ukiwa mafichoni, naita mafichoni kwasababu hakuna anayewaona mkifanya mambo yenu. Mwanamke anaweza kuvaa kimini ambacho kitamfanya mpenziwe asugue sugue vidole vyake kwenye mapaja yake laini bila tabu. Hii itampa msisimko nadhifu ambao unaweza kumfanya akatamani kupanda mlima kilimanjaro ili-afike kileleni. Sehemu ya kifuani, mwanamke anapaswa sehemu baadhi ziwe wazi kumpa mpenzie apate kumtomasa taratibu.
 
Mwanaume nae anaweza kuvaa kaputula ambayo inaweza mwenzie awe huru kumshika sehemu zenye msisimko. Sehemu za kifuani anaweza kuvaa singilandi.
Mtu anapokuwa faragha na mwandani wake hutegemea kupata raha sio karaha.Ukiwa na mwandani ama wamoyo wako, hakikisha huongelei mambo ambayo mlikosana maana katika mapenzi haikosi migogoro midogo midogo.Faragha sio sehemu ya kulaumiana, kama mlishaombana msamaha ya kaisha.Si poa kila mnapokutana kukumbushia maudhi ya mwenzio aliyotubu, kufanya hivyo kutamfanya awe mnyoinge na pengine kluzua majibizano yatakayoondoa Utamu wa mapenzi.
 
Unajua unapokuwa faragha na mwanadani wako, hupaswi kuingiza mawazo ya maisha yako,sijui mimi sina pesa. Mara hiki na kile, kama ni mapenzi basi hakikisheni mawazo yanakuwa kwenye ulingo wa huba.
 
Sasa unafikiri utafanya nini kuhakikisha mwenzako anakuwa na raha ambazo anazitegemea?.
Yapo mambo mengi sana, mfano yawezekana upo kwenye kochi chumbani, mnajiandaa kuelekea nchi ya huba. Unachotakuwa hapo ni nikumthamini mwenzio, ukiwa na kasumba ya dharau hutayafurahia mapenzi yake. Kama hajui mahanjamu mfundishe namna ya kuwajibika. Sio akae kama mzoga huku akikutumbulia macho ya kiburi.
 
Kabla ya kuanza kula tunda, mnapaswa kuhakikisha mmewekana katika hali ya mapenzi, kila mtu awe amesisimka vema, kwani kukurupukia mapenzi ovyo kunaweza kusababisha kutoridhishana. Kwasababu kuna wanaume wengine humaliza kabla ya mwanamke, hivyo kutaka kutoka droo lazima uwe mbunifu na umemwandaa mwenzio vizuri. Pengine anaweza kuniuliza utamwandaa vipi?. Zipo nyingi na pengine hata wewe unazijua, kama kunyonyana ndimi, kutomasana sehemu zenye msisimkona nyingine nyingi ambazo siwezi kuziweka hadharani. Kama unazitaka unaweza kunipigia simu, nitakujulisha.
Utamu wa mapenzi ni kila mtu kujishughulisha mnapokuwa mkipeana mapenzi, haita kuwa vema mmoja anasubiri mwingine ahangaike.

No comments:

Post a Comment