Monday 17 February 2014

Alichosema waziri wa Uingereza kuhusu ujangili nchini

Hili siyo tatizo tu la kimazingira. Kwa tembo 25,000 kuuawa mwaka 2011 na 22,000 kuuawa mwaka 2012, ni ishara inayoonyesha kuwa biashara haramu ya wanyama pori sasa imekuwa ni uhalifu wa kidunia wenye nguvu ya kuathiri maendeleo ya kiuchumi, kusababisha migogoro, kuimarisha vikundi vya kigaidi na kuathiri watu wenye hali duni ya watu waishio katika umaskini.


Tunakabiliwa na janga. Faru wanauawa na maharamia kila baada ya dakika 10 na ni wachache kuliko chui 3,500 ambao wamebaki porini.
Hili siyo tatizo tu la kimazingira. Kwa tembo 25,000 kuuawa mwaka 2011 na 22,000 kuuawa mwaka 2012, ni ishara inayoonyesha kuwa biashara haramu ya wanyama pori sasa imekuwa ni uhalifu wa kidunia wenye nguvu ya kuathiri maendeleo ya kiuchumi, kusababisha migogoro, kuimarisha vikundi vya kigaidi na kuathiri watu wenye hali duni ya watu waishio katika umaskini.
Ujangili unaathiri jamii barani Afrika, hususan yale maeneo katika bara ambapo wanakabiliwa na hali mbaya ya janga la ujangili. Kuna kazi muhimu inaendelea kila siku katika bara zima kushughulikia; kuanzisha jitihada za uhifadhi nchini Namibia au uzoefu wa kiteknolojia mpya nchini Kenya.
Kazi hii imekuwa na athari mbaya kwani zaidi ya askari wa wanyamapori 1000 wamekwisha uawa ndani ya kipindi cha miaka 10 iliyopita. Afrika inaongoza katika mwitikio wa kisiasa kwa hatua zilizochukuliwa katika Mkutano wa Afrika juu ya tembo mwishoni mwa mwezi Desemba mwaka jana (2013) sambamba na jitihada za Gabon katika kuliibua hili katika Umoja wa Mataifa.
Uongozi ulioonyeshwa na Botswana, Gabon na nchi nyingine ndivyo haswa inavyohitajika kulikabili na kulimaliza tatizo.
Lakini ujangili na biashara haramu ya wanyamapori ni suala linaloigusa dunia nzima. Biashara haramu ya wanyamapori ni mtandao wa kutisha wa kiuhalifu ambao una thamani ya mabilioni na ina fursa ya kuyumbisha ukanda na kutishia ustawi wa kimaendeleo endelevu.
Hatupaswi kuiachia Afrika ikabiliane na tatizo hili bila kuwasaidia. Lazima wote tuonje madhara ya uhalifu wa wanyamapori kuanzia usafishaji wa fedha haramu hadi kuharibu mazingira.
Ni jukumu letu kusaidia uongozi ambao nchi za Kiafrika na kwingineno wanaonyesha juu ya suala hili. Hivi karibuni, tumeridhia Mpango Kazi katika Serikali namna ya kukabiliana na biashara haramu ya wanyamapori.
Pia tumetangaza ruzuku mpya za thamani ya paundi milioni 10 kwa miradi ambayo inalenga kukabiliana na ujangili wa tembo na biashara nyingine haramu za wanyamapori na tutatoa taarifa kwa kina baada ya kufahamu mfumo tutakaotumia kutoa ruzuku hizi.
Mnamo Februari 13, Uingereza ilikaribisha Serikali mbalimbali za Afrika, Asia, Amerika na Ulaya kuleta juhudi za pamoja za kimataifa.
Tanzania ilikuwa nchi yenye uwakilishi wa kipekee kwa kuwakilishwa na Rais Jakaya Kikwete, Waziri wa Mambo ya Nje, Benard Membe na Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu. Hili ni jambo lililoleta hamasa na kuonyesha dhamira imara na umakini wa Tanzania katika kushughulikia tatizo la ujangili.
Waziri Nyalandu mnamo Februari 8 mwaka huu (2014) alisema; “Ukizingatia uzito wa tatizo la ujangili linaloikabili Tanzania, Serikali imedhamiria kupambana na kuushinda ujangili”.

 

No comments:

Post a Comment