Wednesday 12 February 2014

ISHARA 10 MUHIMU ZITAKAZO KUONYESHA KWAMBA UKO KATIKA MAPENZI YA KWELI

Hauwezi kuacha kufikiria kuhusu yeye
Muda wote utakua unafikiria kuhusu yeye, kuhusu mipango uliyopanga naye,maisha ya baadae na mengineyo.




Unamjali
Kuna sababu ambazo watu hua hawawaulizi au kuwatafuta wenzao ambao walikutana usiku mmoja na ku-have good time,ni sababu hawajawapenda.Ukiwa in love utataka kujua kila kitu kuhusu mwezako,yeye ni nani,anafikiria nini,  kitu gani kitamfanya afurahi .Unajali kwa ukweli hisia zake.Kama unampenda mtu kweli hautajisikia vizuri anapokua na siku mbaya au tu amekasirika kutokana na jambo fulani.


Ni Mkamilifu
watu wanaopendana huwa wanaangalia mambo mazuri kuhusu wenzao huku wakiyapotezea mapungufu mtu aliyonayo.


unataka akue
Unapotaka mwenzi wako apambane na changamoto mbalimbali ili aweze kukua as a person. Kama unataka mwenzako abaki hivyohivyo na asijaribu vitu vipya basi hapo hamna upendo.


Mna Chemistry nzuri
Hii ni hali ya kufikiria na kutenda kwa upeo mmoja, na kufikiria mawazo yanayofanana au wote kupenda vitu vinavyofanana kama wote kupenda kuogelea,muziki au kusafiri.


Unapenda kutumia muda wako nae
Hii ni jambo lililo wazi lakini ni la muhimu sana.Unasubiri kwa hamu kumuona na kukutana nae huku kutojali kihivyo mtautumiaje muda huo,unachojali ni kuonana nae.Usipokua nae pamoja unam-miss na kutamani angekua nawe.



Unaweza Kuishi na Mapungufu yake
labda ni jasho lake linavyotema akitoka mazoezini au hasira kali aliyonayo anapokasirika na bado ukaweza kukubaliana na hali hii ni ishara tosha ya upendo halisi kwa mwenza wako.


Vipaumbele vingine vinakuja baadae
kawaida unatumia muda fulani kwenda mazoezini lakini anapotaka kwenda dinner basi haitakua tabu kwako kubadilisha ratiba zako na kutoka naye.


Kufanya chochote kwa ajili yake
watu wanaopendana wapo radhi kufanya jambo lolote kwa ajili ya mwenza wako hata kufa kwa ajili yake.


Unaanza kufikiria maisha yako ya baadae na yeye anakwepo
Unapoweza kumuweka kwenye picha yako ya miaka mitano,kumi au hata hamsini mwenza wako basi hiyo ni ishara tosha kwamba unampenda.

No comments:

Post a Comment