Thursday 19 September 2013

Utajuaje kuwa ni "mtendaji mzuri" kitandani?


Habari yako?

Natambua kuna baadhi ya watu hujiuliza kama ni watenaji wazuri kitandani, wengi huamini kuwa "wazuri" kitandani kwa vile wanapenda sana ngono kwa maana ya kuifanya sana, wengine hudhani ni kwasababu wanawaridhisha wapenzi wao.

Baadhi hudai ni watendaji wazuri kitandani kwavile wanauwezo mkubwa wa kingono au kwa kuwa wanakwenda mwendo mrefu bila kuchoka na wengine ni kwasababu wanafanya kila siku.

Ngoni ni sanaa kama zilivyo sanaa nyingine na ili uwe "mzuri" au uweze ku-master inabidi uwe tayari kujifunza na kufanya majaribio ya mara kwa mara, pia unapaswa kuwa mvumiivu kwa maana kuwa ikiwa umejaribu juzi na hukufanikiwa au matokeo hayakuridhisha basi usikate tamaa. Jaribu tena na tena mpaka utakapoweza ku-master unachotaka kukifanya kabla hujarukia kujifunza kitu kipya.

Kwa bahati mbaya hupati Cheti kuonyesha kuwa umefanikiwa na hakuna Jaji/mwalimu atakae kuambia kuwa ume-improve au uongeze nini wapi ili kuwa Bingwa kunako kitanda.

Njia pekee ya kujua uko wapi au umefikia wapi ni kumshirikisha mpenzi wako na kuwa wazi kwake kabla ya tendo(unataka kujaribu nini) wakati (anajisikiaje/unakosea/unapatia) na baada tendo(ilikuaje, nirekebishe nini/wapi)...usimuonee aibu na usijione mjinga au kujishtukia kuwa ni bozo.

Huwezi kuwa mtendaji mzuri kitandani bila kupata ushirikiano kutoka kwa mpenzi wako, vilevie huwezi kuwa mzuri kitandani ikiwa hujiamini kimwili/kimuonekano kwani akili yako itakuwa inafikiria "ulivyo kituko" badala ya kutoa na kupokea wakati wa tendo.

Sasa kabla hujajua kuwa wewe ni mzuri kiutendaji wakati wa kungonoka unapaswa kuzingatia haya kwanza:-

1-Penda, boresha na tunza ulichonacho:

Mwanamke: Ikiwa baada ya watoto 3+ matiti yako yametazama au yanaanza kutazama tumbo then vaa Sidiria kila unapofanya mapenzi. Kama mpenzi anataka kucheza nayo usimuachie akuvue bali mchomolee bila kuivua(ni muhimu kuwekeza kwenye Sidiria na Chupi za maana na kuvutia).

Wake kwa waume: Kama unakitambi au "vishikizo" (minyama-nyama pembezoni mwa tumbo)sio mbaya ukipunguza kwa kubadirisha mtindo wako wa kula na kunywa acha kunywa bia na kwa mwanaume punguza kunywa bia na jitahidi kufanya mazoezi ya kawaida tu kupunguza na kukaza Misuli(sio lazima Gym wala kujinyima chakula).

Mwanamke: Ikiwa kwa bahati mbaya una ile mistari ya unene au baada ya ujauzito au hata kama ni mtumiaji wa Mkorogo lakini sehemu nyingine zikagoma na hivyo kukunyima raha ukiwa Uchi, basi tumia taa ya rangi au mishumaa wakati wa kufanya mapenzi ili kupunguza makali ya mwanga.

2-Amini asemacho mpenzi wako: Kama mpenzi wako anataka kusukuma ngozi ukiwa mtupu kwa vile ndio anavutiwa zaidi basi muamini na ondoa kila kitu na ujiachie.

3-Acha kuibia mwenzio: Kupiga mayowe haikufanyi wewe kuwa "mzuri" kitandani, achia kelele au sauti ikiwa tu ni kweli unasikilizia raha bin utamu....sio ukiguswa tu unatoa ukelele kama vile umefika kumbe hausikii chochote.

Kumbuka mwanaume anajua tofauti za kelele za utamu kwani huambatana na mihemo, unyevu na misuli ya uke kumwenyua-mwenyua(piga ediketa) na zile za wizi kitu kiko vile vile tangu kaingia...so acha wizi.

Wasiliana kwa uwazi: Sema kabla ya tendo nini ungeenda kujaribu, wakati tendo linaendelea uliza mwenzio anajisikiaje na wewe unaeulizwa kuwa wazi kama husikii kitu, unahisi raha n.k....MF: Unajua kuna wakati mnapofanya mapenzi katikati ya tendo unaanza kuhisi kumpenda zaidi mumeo/mkeo sasa ziweke hisia hizo ktk maneno na uziseme...mwambie " nakupenda sana" ile sauti yako ya kutetema kimahaba na mihemo inaweza kukufanya uwe "mtendaji mzuri"...

Ondoa Mipaka: Bibi yangu (Hayati) aliwahi kusema "ukimuwekea mume wako mipaka atakuwa anakuogopa" akimaanisha kuwa atapoteza hamu ya kuendelea na tendo so mipaka ni Mwiko wakati wa kufanya mapenzi.

Pamoja na kusema hivyo Bibi hakuwa na maana kuwa Mume akipeleka uume kwenye O wewe utulie tu aingie...la hasha! aliendelea kwa kusema " Mumeo akitaka kufanya kitu ambacho huna uhakika kama ungependa kufanyiwa au hutaki kufanyiwa unakwepa kimapenzi....sio kukasirika na kususa".

Kama mpenzi wako anataka kujaribu kidole kwenye O yako mwanaume huna haja ya kukasirika na kususa, unatakiwa kushika mkono ule wenye kidole "kimbea"na kuuhamishia eneo lingine ambalo ungependa kushikwa...ikiwa ni mwanamke na uume ndio unasogelea O basi jigeuze huku ukimfanyia mwanaume huyo kitu kingine kimapenzi na ashiki zako zote. Baada ya tendo ndio mwambie mwenzio kuwa usingependa kidole/uume eneo O.

Kila la kheri.

No comments:

Post a Comment