
Lucylight Mallya akizungumzia jinsi alivyojipanga katika masuala ya elimu.
Lucylight ambaye ni mtoto wa kwanza katika familia ya watoto wanne, alisema siri kubwa katika kufaulu kwake ni kufahamu nini anachokitaka katika maisha yake na kuyapenda masomo ya sayansi.
Ni kauli ya mwanafunzi yatima aliyeoongoza kwa ufaulu kidato cha sita
Dar es Salaam. Wakati matokeo 
mengine ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne mwaka jana yakitoka na 
ufaulu kuongezeka, matokeo ya kidato cha sita nayo yametangazwa rasmi 
huku msichana  yatima, akiongoza kitaifa katika kufaulu masomo ya 
sayansi.
 Msichana huyo, Lucylight Mallya (20) alikuwa ni mwanafunzi wa Shule ya Wasichana ya Marian, iliyoko mkoani Pwani.
“Kukosa wazazi kulinifanya nisome kwa bidii zaidi 
kwa kuwa nilijua  kuwa nina majukumu makubwa, maana nina wadogo zangu 
watatu,” alisema Lucylight.  Baba yake alifariki mwaka 2005 na mwaka 
uliofuata akafariki mama yake.
Lucylight ambaye ni mtoto wa kwanza katika familia
 ya watoto wanne, alisema siri kubwa katika kufaulu kwake ni kufahamu 
nini anachokitaka katika maisha yake na kuyapenda masomo ya sayansi.
“Sikuwa nikisoma ili nifaulu mitihani, nilikuwa 
nasoma ili kuelewa kwa kuwa nilifahamu nataka kuwa nani baadaye katika 
maisha yangu,” alisema Lucylight.
Msichana huyo ambaye pia aliongoza katika matokeo 
ya kidato cha nne mwaka 2010, alisema sababu nyingine ya yeye kuwa 
kinara wa masomo ya sayansi nchini, ni kuandaliwa vyema na walimu wake 
na kuiheshimu ratiba yake ya kila siku.
Alisema siku zote aliifuata ratiba ya kujisomea na alipenda zaidi masomo kwa njia ya vitendo kuliko nadharia.
“Unaposoma kwa njia ya vitendo, unalifahamu somo 
zaidi kuliko kwa njia ya nadharia. Ingekuwa shule zote zinafundisha kwa 
vitendo, wanafunzi wengi wangebaini vipaji vyao mapema,” alisema 
Lucylight.
Mwanafunzi huyo mwenye ndoto ya kuwa daktari,  
alilieleza Mwananchi kuwa, huko nyuma  aliyapenda masomo ya biashara 
lakini kwa kuwa alikuwa na uwezo pia katika masomo ya sayansi, walimu na
 wazazi walimshauri ajikite zaidi katika sayansi.
Lucylight, amesoma Shule za Msingi Olimpio na St 
Mary’s zote za jijini Dar es Salaam na  Shule ya Sekondari ya Wasichana 
ya Marian kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita.
Akizungumza na Waandishi wa habari, baba mlezi wa Lucylight,
 Dominic Mallya ambaye ni baba mkubwa alisema mtoto huyo ana kipaji na 
juhudi binafsi.
 
 
 
No comments:
Post a Comment